Makonda kukutana na wabunge wa CCM

DAR ES SALAAM; KATIBU wa NEC Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Paul Makonda amesema atakutana na wabunge wa chama hicho wampe uelekeo wa uenezi wanaotaka wa kistaarabu au wa  vurugu.

Makonda ameyasema hayo leo Oktoba 26, 2023 katika hafla ya kumpokea baada ya kuteuliwa kuwa katibu wa itikadi na uenezi Oktoba 22, 2023 katika Ofisi Ndogo za chama hicho Lumumba jijini Dar e s Salaam.

Amesema: “Nimemuomba Komredi Chongolo Katibu Mkuu wetu na kiongozi wetu, nitaenda nyumbani (Mwanza), nimemuomba kibali chake nitakwenda kumuona Dk. Mwinyi (Rais wa Zanzibar), lakini pia nimemuomba kibali chake nitakwenda kukaa na viongozi wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wabunge wetu ambako ndiko siasa inapikwa, ili waniambie wanataka mwenezi wa namna gani. Mimi naweza kuwa Mwenezi wa aina yeyote. Ni uchaguzi wao.”

Amesema kuteuliwa kushika nafasi hiyo ni kwa mapenzi ya Mungu aliyemfungulia milango akiomba ampe hekima, busara na uvumilivu kukitumikia chama hicho tawala kwa uadilifu.

“Sina maneno mengi nasema asante sana kwa kuwa mtumishi wa wengi, ni matumaini yangu mlango ambao Mungu ameufungua atanipa hekima, busara na uvumilivu na kukitumikia chama kwa uadilifu, uaminifu na mafanikio makubwa ili nisimuabishe Mungu wala Rais aliyeniamini na kuniteua katika nafasi hii,” amesema Makonda.

Ametumia fursa hiyo kuwaomba watumishi wenzake wa chama hicho kumpa ushirikiano na kumshauri.

“Duniani kote watu wanaishi kwa taarifa na taarifa zinafanya uamuzi, ukiwa na chanzo kibovu utafanya uamuzi mbovu, lakini ukiwa na chanzo kizuri utafanya uamuzi sahihi wakati wote,” amesema Makonda akisisitiza kuwa ushirikiano utaifanya CCM kuendelea kuwa na mashiko kwa wananchi.

 

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
4 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Julia
Julia
1 month ago

I’m making over $7k a month working component time. I saved hearing other people inform me how lots cash they could make online so I decided to look at it. Well, it turned into all proper and has definitely modified my life.
.
.
Detail Here————————————————————–>>>  http://Www.BizWork1.Com

Marry
Marry
1 month ago

Surprising! I’ve been making 100 Dollars an hour since I started freelance on the Internet six months ago. I work long hours a day from home and do the basic work that I get from the business I met online. share this work for you opportunity This is definitely the best job I have ever done………


…Go To This Link…………… > > > > http://Www.Smartcareer1.com

Karenray
Karenray
1 month ago

I’ve gained only within four weeks by comfortably working part-time from home. Immediately when I had lost my last business, mtg I was very troubled and thankfully
following website___________ http://Www.Careers12.com

Last edited 1 month ago by Karenray
VITA YA MTU NA RWANDA
VITA YA MTU NA RWANDA
1 month ago

Familia ya bwana MAPIGANO/KUTOKUZIKWA YATANGANZA VITA NA NCHI YA RWANDA YA KUBOMOA DARAJA LA MTO KAGERA PALE RUSUMO  KWA KUTUMIA MABOMU YA KUTENGWA KWA MKONO KWA SIKU 5 LENGO NI KUUWA BIASHARA KATI YA TANZANIA NA RWANDA

Capture.JPG
Back to top button
4
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x