Mambo yamenoga Bwawa la Nyerere

Rais wa Tanzania, Dk Samia Suluhu Hassan leo anatarajiwa kuzindua tukio la kujaza maji katika Bwawa la Julius Nyerere (JNHPP) baada ya ujenzi wake kufikia asilimia 78.68.-

Tukio hilo litakofanyika eneo la mradi, Dk Samia atabonyeza kitufe ambacho kitafunga handaki la kuchepusha maji, hivyo kuruhusu maji kuanza kuingia kwenye bwawa hilo la ujazo wa lita bilioni 32.-

Uzinduzi wa ujazaji maji  ni utekelezaji wa mradi huo ambao utazalisha megawati 2,115 zitakazotosheleza mahitaji ya sasa na kuwa kichocheo cha uwekezaji nchini.-

Advertisement

Taarifa ya Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO, Maharage Chande, imesema kuwa uingizwaji wa maji unatarajiwa kukamilika mwaka 2024, na uzalishaji wa umeme utaanza Juni mwaka huo.

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *