Man United mwaka wa tabu

TIMU ya Manchester United imeaga michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kumaliza kundi A ikiwa na pointi nne, ambazo zimeshindwa kuwavusha kwenda 16 bora.

Katika mchezo wa leo dhidi ya Bayern Munchen ulioisha kwa United kufungwa bao 1-0, timu hiyo ilihitaji ushindi wowote kisha Copenhagen na Galatasaray wamalize kwa sare ila mambo yakawa tofauti baada ya Copenhagen kushinda bao 1-0.

Kwa matokeo hayo, Bayern Munchen imeenda 16 bora ikiwa na pointi 14, na Copenhagen ikiwa na pointi 8.

Advertisement

United ilianza kundi hilo kwa mchezo dhidi ya Bayern ambapo waliofungwa mabao 4-3, kisha wakafungwa tena dhidi ya Galatasaray mabao 3-2.

Mchezo wa tatu dhidi ya Copenhagen, United walishinda bao 1-0, katika mchezo wa marudiano dhidi ya timu hiyo, wakapoteza tena mabao 4-3. United walipata sare ya mabao 3-3 dhidi ya Galatasaray mchezo wa marudiano.

Katika mchezo wa leo, bao la Bayern limefungwa na Kingsley Coman dakika ya 70.

Image Credit: Sky Sport.

13 comments

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *