Mandonga afunika mapokezo Moro

Mandonga afunika mapokezo Moro

BONDIA Karim  Said “Mandoga Mtu Kazi “, amesema kulala vizuri , lishe bora ,  mazoezi  ya nguvu mara kwa mara imemuwezesha kuwa  ni bondia wa kwanza nchini  kupigana mapambano 16 mwaka uliopita.-

Mandoga alisema hayo  mbele ya maelfu ya  wananchi waliojitokeza kupokea eneo la Stendi ya Daladala ya zamani Manispaa ya Morogoro, wakati alipowasili jana  akitokea jijini Dar es Salaam.-

Alisema kuwa mchezo wa ngumi kikanuni bondia anapaswa kucheza  mapambano matatu tu kwa mwaka,  lakini yenye  kutokana na kulala vizuri ,  lishe bora anayoipata na mazoezi ya nguvu kila mara kumemwezesha kucheza mapambano hayo wa  mwaka uliopita.

Advertisement

Alisema kuwa amepata umaarufu na mapokezi makubwa baada ya pambano lake na Mkenya Daniel Wanyonyi  na hiyo ni kutokana na  slogani yake  ya ngumi ya kigeni  anayoiita  Sunguyo, ambayo ni  ya  hatari  iliyomwadhibu bondia huyo Mkenya .

Aliushukuru ubalozi wa Tanzania nchini Kenya kwa kumpa mapokezi mazuri na Serikali ya Awamu ya Sita kwa kumpigania vizuri baada ya kupata ubingwa wake,  ambapo amepokelewa vizuri jijini Dar es Salaam.

 

Mandonga akipongezwa na bondia Twaha Kiduku wakati wa mapokezi hayo (Picha zote na John Nditi).

Aliwashukuru wananchi wa Mkoa wa Morogoroo kwa mapokezi mazuri waliyopatikana pamoja na viongozi wa serikali ya wilaya waliongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Albert Msando.

” Nilikaa na kusikiliza kweli mimi ni yatima niliyokosa baba  na mama , bado sijamaliza kuwaza nikasikia simu Mandonga uko wapi nikajibu viongozi wangu wa Morogoro na kuwambia nipo Dar es Salaam , haraka sana urudi nyumbani kwako Morogoro ndugu zako wote wanakusubiri watu wanataka wakupokee wewe,”alisema Mandonga akielezea mawasiliano kwenye simu yake na viongozi wa Morogoro.

Alimshukuru Mungu kwa kila jambo, ambalo amemfanyia na kumuezesha kupata umaarufu na mapokezi makubwa ya wananchi wa Mkoa wa Morogoro.

Mapokezi makubwa ya bondia huyo yanaendeleza mwendelezo wa kuonesha upendo na kuwajali wasanii na wanamichezo wao, ambapo tukio kubwa lilianza mwaka 2002,  ambapo Mwisho Mwampamba  alikuwa Mtanzania wa kwanza kushinda shindano la Big Brother Afrika Kusini  na alifanyiwa mapokezi makubwa ya heshima.

Mwaka 2004  msanii Selemani Msindi ‘Afande Sele’,  akishinda  ufalme wa Rhymes jijini Dar es Salaam na kupatiwa  zawadi ya gari, aliporudi Morogoro alifanyiwa  mapokezi ya kihistoria.

Mwendelezo  huo ukijitokeza tena mwaka 2008 kwa  Francis Cheka wa Morogoro alishinda mchezo wa ngumi jijini Dar es Salaam dhidi ya bondia mahiri Rashid Matumla .

Mwaka 2020 bondia Twaha Kiduku wa Morogoro alishinda pambano kubwa la ngumi mbele ya Dula Mbabe jijini Dar es Salam, alipewa  zawadi ya gari na kama kawaida aliporudi Morogoro akafanyiwa mapokezi makubwa.

/* */