Mane kumfuata Ronaldo Al Nassr?

KLABU Al Nasrr ya Saudi Arabia  inaelezwa ipo mbioni  kukamilisha uhamisho wa mshambuliaji  Sadio Mane kutoka  Bayern Munich ya Ujerumani

Taarifa zinazoenea katika vyanzo mbalimbali barani Ulaya vinasema kwa sasa yamebaki mazungumzo kati ya Mane na Al Nasrr juu ya maslahi binafsi kwani klabu  zimefikia makubaliano juu ya ada ya uhamisho.

Iwapo dili hilo litakamilika, ni wazi Al Nasrr itakuwa kati ya timu tishio katika Ligi ya Saudia kwani ataungana na wababe wengine kama Cristiano Ronaldo aliyejiunga mwaka jana miongoni mwa nyota wengine wanaosakata kabumbu huko saudi Arabia.

Advertisement

6 comments

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *