Mbadala wa Sonko apatikana uchaguzi Senegal

CHAMA cha kiongozi wa upinzani wa Senegal aliyefungwa jela, Ousmane Sonko kimesema kitamteua mgombea mbadala wa nafasi ya urais katika uchaguzi wa 2024.

Hatua hiyo ni baada ya mahakama nchini humo kutoa uamuzi kuwa kiongozi huyo hatoweza kuwania urais katika uchaguzi ujao.

Chama cha Afrika cha Senegal, Kazi Maadili na Udugu (PASTEF) kimempendekeza Katibu Mkuu wake, Bassirou Diomaye Faye kupeperusha bendera ya chama hicho.

“Kumfadhili mgombea Bassirou Diomaye Faye hakumaanishi kwa vyovyote vile kumsaliti ugombea wa Ousmane Sonko.” Taarifa ya chama alisema.

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *