Mbinu mpya utafiti zahitajika UDSM

CHUO Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kimesema kwa muda mrefu utafiti umekuwa ukifanyika kwa mbinu za kimazoea sasa umefika wakati wa kutafakari mbinu mpya ili kuondokana na mawazo ya ukoloni, kuja na suluhisho kwa matatizo yanayoibuka.

Rasi wa Ndaki ya Sayansi ya Jamii chuoni hapo, Profesa Christina Noe amesema hayo katika ufunguzi wa warsha ya watafiti iliyofanyika chuoni hapo.

Noe amesema katika kutafakari mbinu hizo mpya, Udsm kimeungana na taasisi za nchi tano za kimataifa, ikiwemo Tanzania Sweden yenye vyuo vikuu vitatu, Mali na Burkina Faso.

“Tunafikiria zaidi namna tunavyofanya utafiti kama inatupa matokeo tunayotaka na inatuwezesha kufikiri kwa namna ya uhuru zaidi ili tuwe na matokeo chanya kwa jamii.

“Kupitia mradi huu, tunataka wanafunzi wetu wawe na mbinu za kufanya utafiti chanya ili kutengeneza kizazi cha kufanya utafiti huru,” amesema.

Kuhusu utafiti kufadhiliwa na mataifa tajiri na hatari ya matokeo yake kuathiriwa na matakwa ya wafadhili, alisema pamoja na kuwategemea wafadhili, lakini matokeo ya utafiti hayaathiriwi na watoa fedha kwani duniani kote vyuo vikuu vikiwemo vya Ulaya hutegemea ufadhili kufanya utafiti.

“Mkakati wetu ni kuhakikisha kule fedha zinazotoka kusitufanye sisi kufanya kila wanachotaka. Sisi tuna maeneo yetu, kuna jamii zetu. Kwa hiyo tunatumia fedha bila ya kulazimishwa kufanya kama wanavyotaka,” amesema.

Kwa upande wake mratibu wa kituo cha jamii na dini chuoni hapo kinachoratibu mradi huo, Thomas Ndaluka amesema lengo lake ni kuona kuwa utafiti unaofanyika unakuwa na uhalisia.

“Tumekuwa utafiti mwingi tu huko nyuma, lakini kwa mradi huu tutakwenda mbele zaidi kwa kuangalia njia zitakazoboresha si tu utafiti bali pia jamii tunazoguswa na utafiti. Pia tunalenga kubadili fikra za utafiti na jamii zinazoguswa.

“Tunachosema hakuna anayemiliki ujuzi, ni kitu kinachotakiwa kufanywa kwa pamoja. Unapokuwa na wanafunzi wa uzamili, au uzamivu, inabidi kuwa na njia zinazotengeneza ujuzi wa pamoja. Watafiti wanapokwenda kule kijijini tusiende na mawazo kuwa tuna suluhisho la matatizo yao, kwani wale pia wana njia zao za maisha, bali tuwasikilize wanachosema,” amesema.

Naibu Makamu Mkuu chuoni hapo, Profesa Nelson Boniface aliyemwakilisha Makamu Mkuu wa UDSM, Profesa William Anangisye, amesema ni wajibu wa watafiti kutafuta mbinu mpya za kuondokana na fikra za ukoloni mambo leo na kuangalia uhalisia wa jamii zizilizopo.

Naye Mkuu wa Ushirikiano wa maendeleo wa Ubalozi wa Sweden, Sandra Diesel amesema mwaka huu nchi hiyo inaadhimisha miaka 60 ya ushirikiano na Tanzania ukiwamo ushirikiano katika utafiti.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
4 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Susanames
Susanames
1 month ago

I’ve gained only within four weeks by comfortably working part-time from home. Immediately when I had lost my last business, mtg I was very troubled and thankfully
following website___________ http://Www.Careers12.com

Last edited 1 month ago by Susanames
Royal
1 month ago

[ JOIN US ] I am making a good salary from home 16580-47065/ Doller week , which is amazing under a year ago I was jobless in a horrible economy. I thank God every day I was blessed with these instructions and now it’s my duty to pay it forward and share it with Everyone,
Here is I started.…………>>  http://Www.SmartCash1.com

Last edited 1 month ago by Royal
Marry
Marry
1 month ago

●Im making over $13k a month working part time. I kept hearing other people tell me how much money they can make online so I decided to look into it. Well, it was all true and has totally changed my life.(sl)last month her pay check was $12712 just working on the laptop for a few hours. This is what I do, ↓↓↓↓VISIT THIS WEBSITE↓↓↓↓
HERE☛…..☛ http://Www.Smartcareer1.com

Julia
Julia
1 month ago

Making every month extra dollars by doing an easy job Online. Last month I have earned and received $18,539 from this home based job just by giving this only mine 2 hrs a day. Easy to do work even a child can get this and start making money online.
.
.
Detail Here—————————————————————->>>  http://Www.BizWork1.Com

Back to top button
4
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x