Mbunge ataka bodaboda kunufaika na mikopo

MBUNGE wa Jimbo la Morogoro mjini, Abdulaziz Abood amewataka vijana waendesha pikipiki ( bodaboda ),kuanzisha vikundi na kuvisajili ili wanufaike na mikopo ya fedha zinazotolewa na serikali kwa ajili ya maendeleo yao.

Abood alisema hayo Januari 23,2023  wakati alipotembelea  maeneo mbalimbali ya  vituo  vya kazi vya Bodaboda na kuwakabidhi zawadi za majaketi yenye viakisi mwanga (Reflector Jackets) zipatazo 1,500  yakiwa na ujumbe : “ Sisi na Mama “ na “Tanzania The Royal Tour”.

Advertisement

Mbunge huyo alisema hatua hiyo ni  jitihada za Rais Dk Samia Suluhu Hassan pamoja na yeye (Mbunge ) katika hatua ya kuliepusha kundi hilo kubwa   na ajali  barabarani hususani nyakati za usiku.

Abood  alisema madereva wa bodaboda ni kundi kubwa , hivyo  wakijiunga  kwenye vikundi na kuvisajili watakuwa na uhakika wa kunufaika na fursa za mikopo ya asilimia nne (4) kwa vijana inayotolewa na halmashauri ili kuendeleza kipato chao  kitakachowainua  kiuchumi .

“ Serikali ya awamu ya sita imetoa fursa nyingi za uwezeshaji kiuchumi kwa wanawake , vijana na watu wenye ulemavu , nina waomba vijana tumieni fursa hii , azisheni vikundi vya bodaboda visajilini ili kupata mikopo hii ambayo haina riba “ alisema Abood

Alisema kupitia  mikopo watakayoipata watakuwa na uwezo wa kununua pikipiki za kikundi  vyao na kuendeleza mitaji itakayowaongezea kupata  mafanikio  makubwa ya kijamii na kiuchumi.

“ Azisheni vikundi mimi mbunge wetu nipo  tayari kuwasaidia  kuvisajili , tumieni fursa zinazotolewa na Rais wetu kwani wanawapenda wananchi wake “ alisema Abood

Kuhusu zawadi za majaketi ( Reflector Jackets) Mbunge huyo alisema  licha ya kuwalinda katika usalama wao pia  zina yamebeba ujumbe wa kuitangaza  Tanzania na filamu ya The Royal Tour  kwa vile  wanakutana na watu wa aina mbalimbali wakiwemo raia wa kigeni  na hivyo kufikisha eneo kubwa.

Kwa upande wa madereva hao akiwemo , Ally Yusuph  wa Kituo kikuu cha Msamvu cha Mabasi  yaendayo mikoani alimshukuru Rais  pamoja na Mbunge huyo  kwa jitihada zao za  kulijali kundi hilo .

Yusuph alisema. madereva wengi wa bodabodas  wamefariki dunia kwa kugongwa n magari kutokana na kukosa viasiki mwang hivyo  na upatikanaji wake kwao kutasaidia kupunguza ajali  barabarani hasa  nyakati za usiku na pia kuahidi kutangaza utalii.

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *