UNAAMBIWA Liverpool wako katika hatua nzuri za kumsajili kiungo Alexis Mc Allister kutoka Brighton.
Kwa mujibu wa mwandishi wa habari wa zamani wa Sky Sport, Fabrizio Romano, Liverpool itamalizana na Muagentina huyo mwezi Juni.
Shida nyingine inakuja kwa mujibu wa Gazeti la Mirror nchini Uingereza, Manchester City wameingia kwenye vita hiyo ya kutaka kumsajili mshindi huyo wa Kombe la Dunia.
Hata hivyo haijawekwa wazi kama kuna dau lolote City wamewasilisha kwa Brighton ila Liverpool inabaki kuongoza kwenye mbio za kumsana mkali huyo.