MSHAMBULIAJI wa Inter Miami, Lionel Messi alilazimika kufanyiwa mabadiliko dakika 37 baada ya kupata jeraha katika mchezo wa Ligi Kuu ya Marekani (MLS) ulioisha kwa timu hiyo kushinda mabao 4-0 dhidi ya Toronto FC.
–
Muargentina huyo hakuwepo katika mchezo wa wiki iliyopita ambao Miami ilipochapwa 5-2 na Atlanta.
–
Imeripotiwa kuwa kuna uwezekano nyota huyo akakosa fainali ya Kombe la US Open dhidi ya Houston Dynamo wiki ijayo.
–
Meneja wa Miami, Gerardo Martino alisema mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 36 ana jeraha la zamani hivyo ni kama ametoneshwa.
–
Mshindi huyo mara saba wa Ballon d’Or hakutumiwa na kocha wa Argentina, Lionel Scaloni dhidi ya Bolivia wiki iliyopita.
–
Mchezaji mwenzake wa zamani wa Barcelona, Jordi Alba pia alipata jeraha dhidi ya Toronto na Martino alisema bila shaka wachezaji wote wawili watakosa mchezo wa Jumapili dhidi ya Orlando City.
–
“Hakuna nafasi kwao kwa mchezo wa Jumapili,” Martino alisema. Najua tuna fainali Jumatano lakini hawawezi kucheza.”alisema Martino.


Kaka mchambuzi vipi ubadilike kama Zuwena?
3 comments