Mgodi Kitalu C wageuka shamba la bibi

IMEELEZWA mgodi wa Kitalu C wa Madini ya Tanzanite uliopo Mirerani wilayani Simanjiro mkoani Manyara umekuwa shamba la bibi­­­ baada ya wafanyabiashara wakubwa watatu kuingia katika mgodi huo na kuvuna madini ya mamilioni ya fedha bila hatua yoyote kuchukuliwa.

Mgodi huo unaomilikiwa na serikali na mbia mwekezaji mzawa kampuni ya Franone.

Kampuni tatu zinazodaiwa kuingia Kitalu C na kuchimba kwa njia haramu maarufu kwa njia ya bomu ni pamoja na kampuni ya Tanzanite  Explore inayomilikiwa na Victor Philipo Mkenga na kampuni ya Saniniu Mining inayomilikiwa na Bilionea Saniniu Laizer na Kampuni Manga Gems(T) Ltd  inayomilikiwa na familia ya marehemu Mathias Manga.

Akithibitisha tukio hilo Ofisa Mfawidhi wa Madini Mirerani ,Mernad Msengi alisema ni kweli ofisi yake ina taarifa za tukio hilo na hatua zimeanza kuchukuliwa ikiwa ni pamoja kusimamishwa uchimbaji kwa wafanyabiashara hao waliovamia Kitalu C.

Lakini pia kuwapa nafasi ya mazungumzo kati yao na kampuni ya Franone kabla ya hatua zaidi za kisheria kuchukuliwa dhidi yao.

,,Ni kweli tukio hilo lipo na ofisi yangu imeshachukua hatua ikiwemo kusimamisha uchimbaji kwa kampuni zinazomilikiwa na wafanyabiashara hao kusimama na tumewapa nafasi ya mazungumzo kabla ya hatua zaidi za kisheria kuchukuliwa.” alisema.

Awali tukio lingine liliwahi kutokea Machi 10 hadi 13 mwaka huu kwa kampuni ya Gem Rock Venture inayomilikiwa na mfanyabiashara Joel Mollel maarufu kwa jina la Saitoti kuchimba kwa njia haramu katika kitalu C na kufanya serikali kukosa mapato hivyo hatua zaidi zinahitajika juu ya kuthibiti uchimbaji huo haramu kwa wafanyabiashara wakubwa.

RaisSamia Suluhu Hassan mapema mwaka jana katika hotuba zake aliwahi kuwaonya wafanyabiashara wa Tanzanite kuacha mara moja kuvamia mgodi wa Kitalu C na kuchimba kwa njia ya bomu na kusisitiza kuwa atayekaidi amri hiyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Habari kutoka katika Mirerani zinadai kuwa wafanyabiashara hao walivamia mgodi wa Kitalu C mwanzoni mwa mwezi huu na waliingia zaidi ya mita 600 katika kitalu hicho na kuchimba kwa njia haramu.

Vyanzo vilidai kuwa Saitoti alipochimba kwa njia haramu katika mgodi wa Kitalu C serikali ilimchukua hatua kali ikiwa ni pamoja na kumfungia mgodi wake na pia alifikishwa mahakamani kujibu mshitaka lakini kwa wafanyabiashara hao imekuwa tofauti hivyo kuonyesha wazi kuwa wafanyabiashara hao wanalindwa na baadhi ya vigogo wa serikali kama wanavyotamba wao.

Mkurugenzi wa Manga Gems, Brayan Manga alipoulizwa juu ya tukio hilo alijibu kwa dharau na kusema kuwa hana taarifa za kuvamia kitalu C na kusema kuwa hakuna mtaalamu aliyethibitisha kuwa yeye amevamia mgodi huo.

Mfanyabiashara Victor Mkenga na bilionea Saniniu Laizer kupatikana kuelezea tuhuma hizo kwa kuwa simu zao za kiganjani zilikuwa zikiita bila ya kupokelewa pamoja na kutumiwa ujumbe wa sms mara zote bila ya mafanikio lakini juhudi zaidi zinaendelea kuwasaka.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
8 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Elainloyd
Elainloyd
1 month ago

Single Mom With 4 Kids Lost Her Job But Was Able To Stay On Top By Banking Continuously DOLLER 1500 Per Week With An Online Work She Found Over The Internet… 

Check The Details HERE…..  https://webonline76.blogspot.com/

Last edited 1 month ago by Elainloyd
rofyidilmo
rofyidilmo
Reply to  Elainloyd
1 month ago

My pay at least $300/day.My co-worker says me!I’m really amazed because you really help people to have ideas how to earn money. Thank you for your ideas and I hope that you’ll achieve more and receive more blessings. I admire your Website I hope you will notice me & I hope I can also win your paypal giveaway.
.
.
go to this link_____ https://Fastinccome.blogspot.Com/

JuliaRichard
JuliaRichard
1 month ago

Earn income while simply working online. Work from home whenever you want. Just for maximum 5 hours a day you can make more than $600 per day online. From this I made $18,000 last month in my spare time.
.
.
Detail Here===========================>>>  http://Www.OnlineCash1.Com

CelineEmery
CelineEmery
1 month ago

Make money online from home extra cash more than $18000 to $21000. Start getting paid every month Thousands Dollars online. 6w7 I have received $26000 in this month by just working online from home in my part time. every person easily do this job by.
just copy and paste……………………..>  http://www.SmartCash1.com

Nottingham Forest
Nottingham Forest
1 month ago

Single Mom With 4 Kids Lost Her Job But Was Able To Stay On Top By Banking Continuously DOLLER 1500 Per Week With An Online Work She Found Over The Internet… 
Check The Details HERE…..  https://webonline76.blogspot.com/

Nottingham Forest
Nottingham Forest
1 month ago

TECHNOLOJIA YA UZAZI LEO

INCUBATOR YA KUZALISHA WATOTO WACHANGA WA BINADAMU.
 ✓Inazaliza watoto wachanga 20 kwa wakati mmoja. Huzalisha pia Ng’ombe, Ng’uruwe na Mbuzi. Ina ufanisi mkubwa wa zaidi ya 98% ni full automatic na inageuza mtoto mchanga yenyewe. Ina mfumo rafiki sana kutumia. inatunza joto kwa zaidi ya masaa 75 baada ya umeme kukatika. iko stable na precise kwenye controlling ya joto na unyevu. utapata ofa ya drinker na feeder seti moja bure. ni mpya kabisa.

GHARAMA TSH CENT 1

Nottingham Forest
Nottingham Forest
1 month ago

TECHNOLOJIA YA UZAZI LEO

INCUBATOR YA KUZALISHA WATOTO WACHANGA WA BINADAMU.

 ✓Inazaliza watoto wachanga 20 kwa wakati mmoja. Huzalisha pia Ng’ombe, Ng’uruwe na Mbuzi. Ina ufanisi mkubwa wa zaidi ya 98% ni full automatic na inageuza mtoto mchanga yenyewe. Ina mfumo rafiki sana kutumia. inatunza joto kwa zaidi ya masaa 75 baada ya umeme kukatika. iko stable na precise kwenye controlling ya joto na unyevu. utapata ofa ya drinker na feeder seti moja bure. ni mpya kabisa.

GHARAMA TSH CENT 1

MAPINDUZI.GIF
Najma
Najma
1 month ago

huyu demu aliyecheza na diamond JEJE MZURI SANA ANAPATIKANA MKOA GANI ANATAFUTWA… TUMPE MAUA YAKE ANASTAHILI KUWA NA WAJUKUU 90

OIP.jpeg
Back to top button
8
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x