Mikakati yawekwa upatikanaji  dawa

SERIKALI imesema  inaendelea kuboresha upatikanaji wa dawa na vifaa tiba katika hospitali nchini kwa kutekeleza mambo mbalimbali ikiwemo kuipatia mtaji Bohari ya Dawa ili kuwa na bidhaa za afya muda wote.

Naibu Waziri wa Afya, Dk Godwin Mollel ametoa kauli hiyo bungeni leo, alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Tabora Mjini, Emmanuel Mwakasaka aliyehoji mkakati  uliopo wa kumaliza upungufu wa dawa na vifaa tiba katika hospitali nchini.

“Serikali inaendelea kuboresha upatikanaji wa madawa na vifaa tiba katika hospitali zetu nchini kwa kutekeleza yafuatayo;

“1. Kuipatia mtaji Bohari ya Dawa kwa mwaka wa fedha 2023/2024 ili kuwa na bidhaa za Afya muda, 2. wote. 2. Serikali kutoa fedha za ununuzi wa bidhaa za afya kila mwezi kwa ajili ya vituo vya kutolea huduma za Afya vya Umma.

“ 3. Kuhakikisha suala la usimamizi wa bidhaa za afya linakuwa sehemu ya ajenda ya Kudumu ya Kamati za ulinzi na usalama za wilaya na mikoa.

“4. Kuwasimamia watoa huduma katika vituo vya kutolea huduma za afya ili kuweza kukadiria kwa usahihi. (Forecasting) 5. Vituo vya kutolea huduma za afya kutumia fedha zinazotokana na malipo ya huduma na dawa kununua bidhaa za afya kuliko kutegemea fedha zinazotolewa na Serikali pekee,” amesema Naibu Waziri Mollel.

 

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
3 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Hayleigh Diantha
Hayleigh Diantha
24 days ago

I earn $100 per hour while taking risks and travelling to remote parts of the world. i22 I worked remotely last week while in Rome, Monte Carlo, and eventually Paris. I’m back in the USA this week. I only perform simple activities from this one excellent website.see it,

Click and Copy Here for more info =======>> http://www.SmartCash1.com

Carissa Holman
24 days ago

Our site covers a variety of topics, including digital marketing, business, technology, influencer marketing benefits and more. s Our goal is to provide our readers with insightful and informative content that helps them stay up-to-date on the latest trends and developments in these 
fields Check My Profile Name

Tibirizi Chakechake Pemba
Tibirizi Chakechake Pemba
21 days ago

Hela za kujenga ofisi za serikali zimepungua kwa asilimia 100, manager lini tutasini vifone = ajira zitaongezeka kwa asilimia 300

Capture2.JPG
Back to top button
3
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x