Mikataba 10 yasainiwa kuzalisha ajira 16,355

KITUO cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kimeingia mikataba na kampuni 10 ya uwekezaji wa kimkakati mahiri yenye thamani ya zaidi ya Sh bilioni 1.8.

Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, Ashatu Kijaji alishuhudia utiaji saini mikataba ya uwekezaji huo uliopewa hadhi na Kamati ya Taifa ya Uwekezaji (NISC).

Unatajwa kuwa ni wa kwanza kushuhudiwa na Kituo cha Uwekezaji (TIC) na utatoa ajira za moja kwa moja 16,355 na ajira zisizokuwa za moja kwa moja 200,000.

Akizungumza wakati wa utiaji wa saini wa mikataba hiyo, Kijaji alizitaka taasisi hizo kupunguza na kumaliza changamoto ya Tanzania kuagiza bidhaa kutoka nje wakati uwezo wa kuzalisha upo nchini.

Alisema serikali imekuwa ikiongeza nguvu kwa wakulima, ili waweze kuzalisha malighafi za kutosha zitakazoweza kuchakatwa na viwanda vya nchini na kuzalisha bidhaa zitakazouzwa ndani na nje ya nchi. Kijaji alisema nchi itaondokana na uagizaji wa sukari mwaka 2024.

Alizitaka kampuni za kuchakata mafuta kumaliza kilio cha Watanzania kuhusu uhaba wa mafuta ya kupikia ifikapo mwaka 2027 kwa kuzalisha mafuta tani 560,500 kutoka tani 205,000 zinazozalishwa sasa.

“Haina haja ya kuagiza mafuta kutoka nje, wakati wapo wakulima ambao wanalima mbegu za kukamua mafuta. Kilio cha wawekezaji ilikuwa ni kuwepo kwa viwanda lakini wanakosa malighafi, kwa sasa serikali imewekeza huko tukafanye kazi,” alisema.

Aliongeza kwa kusema serikali itazindua mtandao wa kituo kimoja kwa ajili ya mwekezaji kupata huduma zote sehemu moja, ili kumpunguzia usumbufu wa kutembea na nyaraka kutafuta cheti.

Alisema huduma hiyo itasaidia wageni kuomba vibali na kukamilika kwa siku tatu na haitakuwa na usumbufu kama ambao ulikuwa ukijitokeza mwanzo kutokana na utofauti wa kanuni na kisheria na kufanya baadhi ya wawekezaji kushindwa kuwekeza.

“Nitaendelea kuwaambia kwamba Tanzania si kisiwa kama tupo peke yetu, mwekezaji ukimsumbua anafanya kujadili na kwenda nchi nyingine,” alisema.

Katika kampuni hizo 10 zilizosaini mkataba, sita ni za nje ya Tanzania, tatu ni za wazawa na moja ina ubia na sekta binafsi. Mkurugenzi Mtendaji wa TIC, Gilead Teri alisema tangu kuanzishwa kwa kituo hicho, kwa mara ya kwanza kimeshuhudia utiaji wa saini wa mikataba ya utekelezaji na kampuni 10 kwa wakati mmoja.

Alisema mikataba hiyo inaashiria mafanikio makubwa ya kipindi cha uboreshaji wa mazingira ya uwekezaji, kuongezeka kwa ufanisi wa utoaji wa huduma kwa wawekezaji na kuimarika kwa juhudi za uhamasishaji uwekezaji nchini.

“Tunashukuru wawekezaji walioamua kuungana na juhudi za serikali kuwaletea wananchi maendeleo na kukuza uchumi kupitia uwekezaji,” alisema.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
1 Comment
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Kim
Kim
2 months ago

Make money online from home extra cash more than $18000 to $21000. Start getting paid every month Thousands Dollars online. I have received $26000 in this month by just working online from home in my part time. every person easily do this job.  
….
Open This Website………………>>>  http://www.Richcash1.com

Last edited 2 months ago by Kim
Back to top button
1
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x