Miti ya asili, pombe za kienyeji kudhibiti wadudu kwenye kahawa

DAR ES SALAAM: VIUATILIFU vya asili visivyo na kemikali pamoja na mitego inayotumia vileo vya kienyeji vimeweza kudhibiti wadudu waharibifu wa kahawa aina ya mapembe, kimatira na ruhuka.
Mtafiti kutoka Taasisi ya Utafiti wa Kahawa Tanzania (TaCRI), Dk Leonard Kiwelu ameelezea hayo kama mchango wa sayansi, teknolojia na ubunifu katika maendeleo ya kiuchumi na kijamii hapa nchini.
Amesema taasisi hiyo ilifanya utafiti na kugundua viuatilifu hivyo vya asili ambavyo vinatumia mimea ya utupa na mwarobaini vina uwezo wa kudhibiti wadudu hao, ikiwa ni mbadala wa matumizi ya ‘frofenoros’ ambayo imezuiliwa kutumika kwenye kahawa.
Ametaja aina za pombe za kienyeji zinazotumika katika mitego hiyo kuwa ni mbege, dengulua, ulanzi na rubisi ambazo zimekuwa chambo cha kuwatega wadudu hao waharibifu wa kahawa.
Amesema tayari bustani 12 zenye miti hiyo ya viuatilifu aina ya utupa na mwarobaini zimeanzishwa katika wilaya ya Hai maeneo ya Shari na Uswaa.
Pia wilaya ya Moshi Vijijini mashamba hayo yameanzishwa katika eneo la Mrimbo, Uuwo na Mawanjeni, pamoja na wilaya za Lushoto, Mwanga, Rombo na Arumeru.
Ameeleza kuwa katika tafiti hizo imebainika kuwa ili mkulima wa kahawa apate faida anapaswa kuwa na angalau miti 450 ya kahawa, kila mmoja ukiwa na matawi ya msingi 25 hadi 45 yenye uwezo wa kuzaa.
Single Mom With 4 Kids Lost Her Job But Was Able To Stay On Top By Banking Continuously DOLLER 1500 Per Week With An Online Work She Found Over The Internet…
Check The Details HERE….. https://smartcareer12.blogspot.com/
I’m making $90 an hour working from home. I never imagined that it was honest to goodness yet my closest companion is earning 16,000 US dollars a month by working on the connection, that was truly astounding for me, she prescribed for me to attempt it simply. Everybody must try this job now by just using this website… http://Www.Smartwork1.Com