MKOJO wa sungura ukivundikwa kwa siku saba unaweza kutumika shambani kwa ajili ya kufukuza wadudu waharibifu kupitia harufu yake.
Ofisa kutoka Shirika la Agri Connect kwenye mradi unaosimamia na kutoa elimu ya kilimo cha mazao ya mbogamboga, matunda, kahawa na chai, Innocent Makura ameeleza hayo katika maonesho ya Nanenane kiitaifa yanayoendelea mkoani Mbeya.
Amesema mkojo huo wa sungura pia unatumika kama mbolea.