Mlango mkuu waenda kwa miguu Muhimbili wafungwa

HOSPITALI ya Taifa ya Muhimbili(MNH), imetangaza kufunga lango  kuu la kuingilia  kwa waenda kwa miguu kwa muda wa miezi mitatu kuanzia Desemba 12 ,2022, hadi Machi 30,2023, ili kupisha ukarabati wa eneo hilo.

Taarifa iliyotolewa na Kaimu Mkuu Kitengo cha Uhusiano wa Hospitali hiyo, Neema Mwangomo, imesema kufuatia hatua hiyo, wananchi watakaofika  hospitalini wanashauriwa  kutumia geti la kutokea  lililokaribu na jengo la wazazi.

“Tunapenda kuwatangazia wananchi wote kwamba tunafunga lango kuu la kuingilia hospitali kwa waenda kwa miguu kwa miezi mitatu,”amesema.

Advertisement

Mwangomo ameeleza kuwa wananchi pia watatakiwa kutumia geti la kuingia chuo kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi (MUHAS), lakini wanaotumia magari kuingia hawataathirika na ufungaji huo.

“Tunaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza ,tunaomba ushirikiano wenu ,”amesisitiza

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *