Mlipuko wauwa watu 57 Pakistan

WATU 57 wameuawa na wengine 60 kujeruhiwa katika shambulizi la kujitoa muhanga karibia na eneo lenye misikiti miwili wakati wa muendelezo ya sherehe za kuzaliwa kwa Mtume Muhammad, nchini Pakistan, qReuters wameripoti.

Imeelezwa hakuna kundi lililodai kuhusika na milipuko hiyo.

Vyombo vya habari mbalimbali duniani vinaripoti kuwa kuongezeka kwa mashambulizi ya wanamgambo kumeongeza hatari kwa vikosi vya usalama kabla ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Januari.

Mlipuko wa kwanza, katika Mkoa wa Kusini magharibi wa Balochistan, uliua watu 52, kulingana na afisa wa afya wa wilaya, Abdul Rasheed.

“Mshambuliaji alijilipua karibu na gari la polisi karibu na Msikiti wa Madina ambapo watu walikuwa wakikusanyika kwa maandamano,” aliongeza afisa mkuu wa polisi Munir Ahmed.

Shambulio la pili katika eneo jirani la Khyber Pakhtunkhwa kaskazini-magharibi liliua watu watano kwenye msikiti mmoja, kwa mujibu wa maafisa wa uokoaji. Paa la msikiti liliporomoka, mtangazaji wa Geo News alisema, na kuwakandamiza takriban watu 30 hadi 40 chini ya vifusi.

Shambulio hilo lilihusisha milipuko miwili, mmoja ukiwa kwenye lango la msikiti na mwingine katika boma hilo, afisa mmoja alisema.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
1 Comment
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
AnneSmith
AnneSmith
2 months ago

Earn income while simply working online. work from home whenever you want. just for maximum 5 hours a day you can make more than $600 per day online. From this I made $18,000 last month in my spare time.
.
.
Detail Here——————————————————>>>  http://Www.BizWork1.Com

Back to top button
1
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x