Mount akaribia Old Trafford

KIUNGO mshambuliaji wa Chelsea, Mason Mount anafanyiwa vipimo vya afya muda huu katika uwanja wa mazoezi wa Carrington kwa ajili ya kujiunga na Manchester United.
Taarifa iliyotolewa na mwandishi wa habari za michezo nchini Italia, Fabrizio Romano imeeleza kuwa Mwingereza huyo atasaini mkataba wa miaka mitano utakaomuweka Old Trafford hadi mwaka 2028 wenye kipengele cha kuongeza mwaka mmoja mpaka Juni 2029.
United inapanga kumtangaza mchezaji huyo kama usajili wao kwanza mara baada ya vipimo na mipango ya mwisho kwenda sawa.
Mount atakamilisha dili huo kwa ada ya uhamisho wa £55m pamoja na ongezeko la £5m.
My last paycheck was $2500 for working 12 hours a week online. My sisters friend has been averaging 8k for months now and she works about 30 hours a week. I can’t believe how easy it was once I tried it out. The potential with this is endless.
…
This is what I do……….>>> https://goodfuture10.blogspot.com