Mtama watakiwa kuepuka chuki za kisiasa

MBUNGE wa Jimbo la Mtama mkoani Lindi, ambaye pia ni Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye, amesema jamii ijielekeze katika kufanya kazi za maendeleo badala ya chuki za kisiasa.
Ametoa kauli hiyo alipokuwa akizungumza na wakazi wa jimbo hilo katika Ofisi ya Mbunge wa Mtama na kusisitiza kuwa kipindi hiki hasa kwa vijana ni cha kufanya kazi kujipatia maendeleo ya kiuchumi.
Amesema si vyema kila kukicha watu kukaa vijiweni na kujengeana chuki za vyama vya CCM na Chadema, huku viongozi wa ngazi za juu wa vyama hivyo wanazungumza wakati wananchi wa kawaida wanajengeana chuki na maneno yasiyofaa.
Pia amewataka vijana kuchangamkia fursa katika mgosi wa Nammangale utakapoanza kufanya kazi mwakani, baada ya kukamilika kulipwa fidia kwa wanainchi waliopisha mradi.
Make money online from home extra cash more than $18000 to $21000. Start getting paid every month Thousands Dollars online. I have received $26000 in this month by just working online from home in my part time. every person easily do this job by.
…
Just Open This Website………>>> http://www.Richcash1.com