Mtendaji Mkuu Man United kuachia ngazi

BREAKING: MTENDAJI Mkuu wa Manchester United, Richard Arnold ataondoka katika nafasi hiyo mwishoni mwa mwaka huu, BBC Sports imeripoti.

Mhasibu huyo mwenye umri wa miaka 52 alichukua nafasi ya Ed Woodward kama mtendaji mkuu wa United mnamo Februari 2022.

Kuondoka kwake, ambako bado hakujathibitishwa rasmi, kunakuja wakati Kampuni ya INEOS Group ya Sir Jim Ratcliffe ikijiandaa kukamilisha ununuzi wa asilimia 25 ya hisa za klabu hiyo.

Mkataba huo unatarajiwa kupitishwa katika kipindi cha mapumziko ya kimataifa mwezi huu.

2 comments

Comments are closed.

/* */