Museveni apona uviko-19

Rais wa Uganda, Yoweri Museveni ametangaza kupona maambukizi ya UVIKO-19.
Hatua hiyo ni baada ya Juni 07, 2023 kiongozi huyo kutangaza kuwa na maambukizi ya UVIKO-19, baada ya siku 11 za kujitenga hatimaye amepima na kupata majibu ya kuondokana na janga hilo.
Museveni amewataka Wananchi wa Uganda kufuata maelekezo ya wataalamu wa afya ya namna ya kujikinga na ugonjwa huo.