Mwanahabari akemea matukio ukatili kwa watoto

MWANAHABARI mtetezi wa watoto na wanawake, Dk Tumaini Msowoya amelaani matukio ya kikatili dhidi ya watoto likiwemo la hivi karibuni mjini Iringa lililomuhusisha baba kumnyonga mwanaye huku akijirekodi video.

Baba huyo, Goodluck Mgovano (35) mkazi wa mtaa wa Kota kata ya Mlandege mjini Iringa anatuhumiwa kumuua mtoto wake wa miaka minne kwa kumnyonga kwa kamba ya viatu huku akirekodi tukio hilo la kinyama kwa simu yake ya mkononi na kisha kuacha ujumbe mfupi wa maandishi kuelezea chanzo cha mauaji hayo na wapi angetamani mwili wa mtoto huyo uzikwe.

Dk Msowoya ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya Siasa Mkoa wa Iringa alisema; “Watoto ni waathirika wasio na hatia wa matukio haya ya ukatili hivyo wanapaswa kulindwa na kulelewa kwa upendo na heshima.”

Akizungumza na mamia ya waumini wa Kanisa Katoliki, Kigango cha Mbigili wakati akimuwakilisha Mbunge wa Jimbo la Kilolo, Justine Nyamoga kwenye uzinduzi wa Albamu ya Kwaya ya Mt Augustino, Dk Msowoya alisema:

“Ukandamizaji, unyanyasaji wa kimwili, kijinsia, kisaikolojia, au unyanyasaji wa kihisia kwa watoto ni makosa makubwa na yanapaswa kuchukuliwa hatua za kisheria.

Alisema kila mtu ana wajibu wa kutoa usalama na ulinzi kwa watoto na kushirikiana na mamlaka husika kutoa msaada kwa waathirika na kuzuia matukio ya ukatili dhidi ya watoto.

“Watoto wanapaswa kuwa na mazingira salama na yenye upendo ili waweze kukua na kufanikiwa katika maisha yao,” alisema na kuwaomba wananchi pamoja na viongozi wa dini zote kuzungumza na kukemea matukio haya ya ukatili yanayo utia doa mkoa wa Iringa.

“Hii ni hatari, wakati Rais Samia Hassan Suluhu anapambana kuboresha miundo mbinu ya elimu, watoto wanafanyiwa ukatili bila huruma. Sasa tuseme basi,” alisema.

Katika tukio hilo, kwaya ya Mt Augustino wamefanikiwa kuzindua albamu yao ya kwanza yenye nyimbo nane ikibeba jina la Enyi watu wa Mataifa.

Viongozi mbalimbali akiwemo Diwani wa Kata ya Lugalo na Nyalumbu walihudhulia uzinduzi huo ambao ulikusanya zaidi ya kwaya 10 kutoka madhehebu mbalimbali.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
3 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
POLISI
POLISI
1 month ago

UNAKARIBISHWA KWENYE UJENZI WA JIJI BILA VITU VIFUATAVYO KUWEPO (ZINAHITAJI WATU WENGI SANA AMBAO HAWAPO DUNIANI):-
–        POLISI
–        BAR
–        LODGE/HOTEL
–        CASINO
–        KANISA
–        MSIKITI
–        SOKO/SHOPPING MALLS
–        SHULE
–        HOSPITALI
–        BARABARA ZA MTAA
–        VYUO
–        FEMU ZA DUKA
–        Makapuni ya Mtandao wa SIMU/BENKI

KWA JINA LA BABA NA LA MWANA NA LA ROHO MTAKATIFU
BWANA YESU ASIFIWE

P – STAND FOR PROPERTY
L – STAND FOR LAND

Capture.JPG
POLISI
POLISI
1 month ago

UNAKARIBISHWA KWENYE UJENZI WA JIJI BILA VITU VIFUATAVYO KUWEPO (ZINAHITAJI WATU WENGI SANA AMBAO HAWAPO DUNIANI):-
–        POLISI
–        BAR
–        LODGE/HOTEL
–        CASINO
–        KANISA
–        MSIKITI
–        SOKO/SHOPPING MALLS
–        SHULE
–        HOSPITALI
–        BARABARA ZA MTAA
–        VYUO
–        FEMU ZA DUKA
–        Makapuni ya Mtandao wa SIMU/BENKI

KWA JINA LA BABA NA LA MWANA NA LA ROHO MTAKATIFU
BWANA YESU ASIFIWE…

P – STAND FOR PROPERTY
L – STAND FOR LAND

Capture.JPG
Angila
Angila
1 month ago

HOME-BASED real Earner.I am just working on Facebook only 3 to 4 hours a Day and earning $47786 a month easily, that is handsome earning to meet my extra expenses and that is really life changing opportunity.(Qf) Let me give you a little insight into what I do…

FOR More Details……….. >> http://Www.Smartcareer1.com  

Back to top button
3
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x