Mwenge waingia Kagera

Mwenge waingia Kagera

MWENGE wa Uhuru umeingia mkoani Kagera, ambapo kilele chake itakuwa Oktoba 14 mwaka huu na mgeni rasmi atakuwa Rais Samia Suluhu Hassan.

Makabidhiano ya Mwenge wa Uhuru yamefanyika katika Kijiji cha Nyamigere, Wilaya ya Biharamulo, mkoani Kagera, ambapo <kuu wa Mkoa wa  Kigoma,  Thobias Andengenye, alimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Mkoa wa  Kagera,  Albert Chalamila Mwenge huo wa huuru.

Kwa mujibu wa Chalamila mwenge huo ukiwa mkoani Kagera utazindua, kukagua na kuweka mawe ya msingi katika miradi  ya maendeleo 37 yenye thamani ya  Sh Bilioni 13.

Advertisement

Baada makabidhiano hayo, Mkuu wa Mkoa wa Kagera, alikabidhi Mwenge huo kwa Mkuu wa Wilaya ya Biharamulo, Kemilembe Rwota.

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *