Mwenye ulemavu wa macho aja kivingine kwenye teknolojia

DSM; KIJANA Malick Hamis (24) mwenye ulemavu wa macho amebuni mfumo wa kupakua sauti kwa kutumia kompyuta na kuziunganisha, jambo linaloonesha kukua kwa teknolojia kwa makundi mbalimbali katika jamii.

Akizungumza leo Dar es Salaam katika kongamano la saba la TEHAMA (TAIC), lilioandaliwa na Tume ya Tehama nchini (ICTC), Malick alisema lengo lake ni kubobea katika suala zima la ubunifu kwenye Tehama.

Amesema alianza matatizo ya macho akiwa darasa la tatu na katika harakati za kufuatilia matibabu alishindwa kumaliza darasa la saba na kuishia la sita.

” Licha ya kutomaliza shule lakini nilisikia taarifa kuwa mtu asiyeona anaweza kupata elimu ,” amesema na kuongeza kuwa ndipo alipojiunga na elimu saidizi inayotolewa na Chuo Kikuu Huria (OUT) na kuanza masomo mwaka 2019.

Amesema aliendelea kusoma masuala ya kompyuta na mwaka huu 2023 alihitimu na kupewa vyeti.

Amesema pamoja na kuwa na ubunifu wa kuunganisha sauti, lakini pia anajifunza kutumia kompyuta kuhariri (editing)katika nyanja balimbali na katika kupakua mfumo wa sauti amepakua sauti za baadhi ya viongozi wakuu wa serikali.

Kwa upande wake Faraja Mwansasu ambaye naye ni mlemavu wa macho ameisihi serikali kuhakikisha kuwa na vifaa jumuishi kwa kundi hilo.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
1 Comment
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Work At Home
Work At Home
1 month ago

Cash generating easy and fast method to work part time and earn an extra $15,000 or even more than this online. By working in my spare time I made $17990 in my previous month and I am very happy now because of this job. you can try this now by following 

the details here…… http://Www.Smartcash1.com

Last edited 1 month ago by Work At Home
Back to top button
1
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x