Mwigizaji Urusi afariki mbele ya wanajeshi Ukraine

MWIGIZAJI raia wa Urusi, Polina Menshikh ameuawa katika tukio la mlipuko wakati akifanya onesho mbele ya vikosi vya jeshi nchini Ukraine. BBC imeripoti.

Tukio hilo limetokea November 19, imeelezwa Polina alialikwa kutoa burudani katika siku ya mapumziko ya vikosi vya jeshi la Ukraine.

Taarifa za vyombo vya habari nchini humo zinasema tukio hilo limetokea eneo la ukumbi wenye uwezo wa kubeba watu 150.

Shirika la Habari Uingereza (BBC) limesema limezungumza na msemaji wa jeshi la Ukraine kupitia idhaa ya BBC ya Ukraine, ambapo alithibitisha tukio hilo.

4 comments

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *