Mzee Mwinyi afariki Dunia akiwa na miaka 98

Rais Samia Suluhu Hassan ametangaza siku saba za maombolezo Mzee Mwinyi alikuwa akisumbuliwa na saratani ya mapafu

Rais Mstaafu wa awamu ya pili wa Tanzania, Ali Hassan Mwinyi amefariki Dunia leo Februari 29, 2024 majira ya saa 11:30 jioni katika Hospitali ya Mzena, Jijini Dar es Salaam alipokuwa akipatiwa matibabu ya ugonjwa wa saratani ya mapafu.

Rais Samia Suluhu Hassan ametangaza kifo cha kiongozi huyo aliyewahi kuwa Makamu wa Rais, Rais Zanzibar na Rais wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kipindi cha miaka 10, kuanzia mwaka 1985 hadi 1995.

 

Advertisement

View this post on Instagram

 

A post shared by Dr Hussein Ali Mwinyi (@dr.hmwinyi)

Mzee Mwinyi amekuwa akipatiwa matibabu tangu November 2023 London Uingereza na baadaye kurejea nchini na kuendelea na matibabu Jijini Dar es Salaam.

Rais Samia ametangaza siku saba za maombolezo kuanzia kesho Machi 1. Mzee Mwinyi atazikwa Unguja, Machi 2, 2024.