NASA yabainisha maeneo 13 kutua mwezini

NASA imetangaza kuwa imechagua maeneo 13 yaliyoko katika ncha ya kusini mwa Mwezi ambayo yatatumika kama vituo vya wanaaga wa Artemis III, mradi unaotazamiwa kupeleka tena wana anga Mwezini mnamo 2025.

“Kuchagua maeneo haya kunamaanisha kuwa tumekaribia kuwarejesha wanadamu Mwezini kwa mara ya kwanza tangu Apollo,” alisema Mark Kirasich, Naibu msimamizi wa Idara ya Maendeleo ya Kampeni ya Artemis katika Makao Makuu ya NASA huko Washington.

NASA ilisema kila eneo moja liko ndani ya digrii sita za latitudo ya Ncha ya Kusini ya mwandamo, eneo la barafu ya maji inaaminika kuwa katika volkeno zenye kivuli cha kudumu na inaweza kutoa ufikiaji endelevu wa jua katika kipindi cha siku 6.5, muda uliopangwa wa Ujumbe wa Artemis III.

Misheni za Apollo zilifanyika zaidi ya miaka 50 iliyopita zilienda katika maeneo ya ikweta ya Mwezi, ambapo kuna sehemu ndefu za mchana, kwa muda wa wiki mbili. Ncha ya Kusini inaweza kuwa na siku chache tu za mwanga, na kufanya misheni kuwa na changamoto zaidi.

“Maeneo kadhaa yaliyopendekezwa yapo kati ya sehemu kongwe zaidi za Mwezi, na pamoja na maeneo yenye kivuli cha kudumu, hutoa fursa ya kujifunza juu ya historia ya Mwezi kupitia vifaa vya mwandamo ambavyo havijasomwa hapo awali,” alisema Sarah Noble wa Artemis anayeongoza Kitengo cha Sayansi ya Sayari cha NASA.

Ufikiaji wa rasilimali ya barafu na mwanga wa jua ni muhimu kwa kukaa kwa muda mrefu Mwezini kwa sababu hutoa chanzo cha nishati na kupunguza tofauti za halijoto. Tofauti na misheni ya Apollo iliyohitimishwa mnamo 1972, Artemis imeundwa kuunda uwepo wa kudumu ndani na karibu na Mwezi.

 

Habari Zifananazo

Back to top button