Ndalichako aagiza mafunzo sekta zisizo rasmi

WAZIRI wa Nchi ,Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana , Ajira na Wenye Ulemavu, Profesa Joyce Ndalichako ameuelekeza Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi  (OSHA) kwa kushirikiana na wadau wengine kuendelea kutoa mafunzo katika sekta isiyorasmi.

Ameutaka wakala huo kutenga bajeti itakayotumika katika utoaji wa mafunzo na elimu endelevu kwa kushirikiana wadau katika sekta isiyorasmi ambayo imeonesha kuadhirika zaidi ya ajali na vifo sehemu  za kazi.

Profesa Ndalichako ametoa agizo hilo Aprili 28, 2023  katika kilele cha Maadhimisho ya siku ya Usalama na Afya  Duniani ambayo kitaifa imefanyika  mkoani Morogoro.

Waziri Profesa Ndalichako amesema  kwa  bahati mbaya  katika sekta isiyo rasmi wanafanya kazi katika mazingira magumu na mara nyingi  hata huduma za ukaguzi  mahala pa kazi haziwafikii kwa kiwango kinachotakiwa .

Profesa Ndalichako amesema  kwa sasa hakuna mfumo ambao ni rasmi uliaondaliwa kuripoti ajali na magonjwa yanayotokea katika sekta isiyorasmi ,na hivyo ina kuwa ni vigumu kufahamu takwimu kwa uhakika na hali halisi ya usalama na afya katika sekta hiyo.

“ Nichukue nafasi hii katika maadhimisho haya ya Usalama na Afya  Duniani kuwaelekeza  Osha kwa kushirikiana na wadau wengine kuendelea kutoa mafunzo  katika sekta hii isiyorasmi” amesema  Profesa Ndalichako

Waziri hiyo amesema  kuwa mafunzo hayo yawe ni endelevu na sio kusubiri wakati wa maadhimisho ya siku ya Usalama na Afya  Duniani  na ili kufanikisha lengo hilo , Wakala huo haina budi  kutenga bajeti ya kuwafikia wafanyakazi  katika sekta isiyo rasmi.

“ Kama mlivyofanya safari hii mmetoa  mafunzo kwa Wajasiliamali 3,748, lakini iwe ni endelevu na mtenge  na bajeti “ amesma  Profesa Ndalichako

Waziri  Profesa Ndalichako amesema , Ofisi yake isingependa kuona mfanyakazi iwe katika sekta rasmi au sekta isiyo rasmi anapata madhara anapokuwa kazini .

Profesa Ndalichako amewataka  wadau kuunga mkono jitihada za Rais Dk Samia Suluhu Hassan ambaye amekuwa akiendelea kuzalisha ajira kupitia sekta ya Umma na amekuwa akiendelea kuimarisha sekta binafsi ambayo inazalisha ajira kwa Watanzania .

“ Tumuunge mkono kwa kuhakikisha ya kwamba tunaweka amzingira ambayo yatalenga kupunguza au kundoa ajali na vifo vinavyotokana na kazi” amesema  Profesa Ndalichako

Profesa Ndalichako amesema  kwa pamoja kama Taifa  tutaweza kuwa na  suluhisho la matatizo ya usalama na afya mahali pa kazi endapo  watafanya kazi kwa ushirikiano .

Hivyo amezotaka   mamlaka za utatu pamoja na waajiri kuendelea kuimarisha mifumo ili kuendelea kulinda nguvu kazi ya Tanzania .

Profesa Ndalichako amesema  serikali inaendelea  kuthamini na kutambua juhudi za taasisi za umma na binafsi zinavyojituma katika kuboresha mazingira  ya kazi na kwa wafanyakazi wao bila kushurutishwa .

“ Sheria zipo lakini tunafurahi tunapoona watu wanatii sheria bila shuruti “ amesema  Profesa Ndalichako

Amesema  serikali itaendelea kuhakikisha ya kwamba kusimamia  usalama na afya mahali pa kazi  na aliwakumbusha waajiri kuzingatia  kauli mbiu yam waka huu “ Mazingira Salama na Afya  ni Kanuni na Haki ya Msingi Mahali pa Kazi”.

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button