Kiongozi wa Israel, Benjamin Netanyahu ameidhinishwa kuwa Waziri Mkuu wa Israel baada ya baraza lake la mawaziri lenye misimamo mikali ya mlengo wa kulia likiapishwa kwa ahadi za kupanua makaazi ya walowezi wa Kiyahudi katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu na kufuata sera nyingine zinazokosolewa ndani na nje ya nchi.
Kiongozi huyo mkongwe, 73 anayekabiliwa na mashtaka ya ufisadi anayokanusha, ametaka kutuliza wasiwasi kuhusu hatima ya haki za kiraia na diplomasia tangu kambi yake ya vyama vya kitaifa na kidini kupata wingi wa wabunge katika uchaguzi wa Novemba 1.
Washirika wake ni pamoja na vyama vya Uzayuni wa Kidini na Vyama vya Nguvu za Kiyahudi, ambavyo vinapinga utawala wa Palestina na viongozi wake walowezi wa Ukingo wa Magharibi – hapo awali walichochea dhidi ya mfumo wa haki wa Israel.
Chama cha kihafidhina cha Netanyahu cha Likud kilisema katika miongozo yake kwa serikali kwamba “kitakuza na kuendeleza makazi” kwenye ardhi ambayo “watu wa Kiyahudi wana haki ya kipekee na isiyoweza kupingwa”.
Mataifa mengi yenye nguvu duniani yanaona kuwa makazi yaliyojengwa kwenye ardhi iliyotekwa vitani ni kinyume cha sheria.
“Miongozo hii ni ongezeko la hatari na itakuwa na athari kwa eneo,” alisema Nabil Abu Rudeineh, msemaji wa Rais wa Palestina Mahmoud Abbas, alisema.
Netanyahu, ambaye sasa anaingia katika muhula wake wa sita, anasema atatumikia Waisraeli wote. Pia anaonekana kuacha kutaka kunyakuliwa katika Ukingo wa Magharibi – sera ambayo alikuwa ameipigia debe hapo awali na ambayo ingefurahisha kambi yake ya walowezi wakati akiiweka Israel kwenye mkondo wa mgongano na Washington na mataifa ya Kiarabu.