Neymar aumia tena

DARWIN Nunez na Nicolas De la Cruz wameipa Uruguay ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Brazil, mchezo wa kufuzu Kombe la Dunia 2026 jana, huku Neymar akilazimika kuondolewa kipindi cha kwanza baada ya kuumia kifundo cha mguu.

Nunez alianza kufunga dakika ya 42 kwa mpira wa kichwa na usiku wa Brazil ukazidi kuwa mbaya dakika mbili baadaye Neymar aliumia wakati akigombea mpira na De la Cruz.

Akiwa na huzuni, Neymar aliondoka uwanjani kwa machela baada ya kupokea matibabu kwa dakika kadhaa.

FA ya Brazil ilisema kuwa fowadi huyo alikuwa na maumivu mkali ya goti la kushoto na kwamba atafanyiwa vipimo ili kubaini kama kuna shida zaidi.

“Hebu tutumaini sio jambo kubwa,” nahodha wa Brazil Casemiro aliambia televisheni ya Globo.

“Ni mchezaji muhimu kwetu, tunampenda sana. Amekuwa akisumbuliwa sana na majeraha na anapoanza kurudi kwenye uwezo wake anaumia tena.”

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
1 Comment
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Work AT Home
Work AT Home
1 month ago

I am creating an honest wage from home 1900 Dollars/week , that is wonderful, below a year gone i used to be unemployed during an atrocious economy. I convey God on a daily basis. I used to be endowed with these directions and currently it’s my duty to pay it forward and share it 

with everybody…. http://Www.Smartcash1.com

Last edited 1 month ago by Work AT Home
Back to top button
1
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x