DARWIN Nunez na Nicolas De la Cruz wameipa Uruguay ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Brazil, mchezo wa kufuzu Kombe la Dunia 2026 jana, huku Neymar akilazimika kuondolewa kipindi cha kwanza baada ya kuumia kifundo cha mguu.
–
Nunez alianza kufunga dakika ya 42 kwa mpira wa kichwa na usiku wa Brazil ukazidi kuwa mbaya dakika mbili baadaye Neymar aliumia wakati akigombea mpira na De la Cruz.
–
Akiwa na huzuni, Neymar aliondoka uwanjani kwa machela baada ya kupokea matibabu kwa dakika kadhaa.
–
FA ya Brazil ilisema kuwa fowadi huyo alikuwa na maumivu mkali ya goti la kushoto na kwamba atafanyiwa vipimo ili kubaini kama kuna shida zaidi.
–
“Hebu tutumaini sio jambo kubwa,” nahodha wa Brazil Casemiro aliambia televisheni ya Globo.
–
“Ni mchezaji muhimu kwetu, tunampenda sana. Amekuwa akisumbuliwa sana na majeraha na anapoanza kurudi kwenye uwezo wake anaumia tena.”


1 comments