ILI kuwalinda wananchi wanaosafiri nje ya nchi na majanga ya dharura, NIC Insurance, imetambulisha bima ya Safari ambayo mteja anayesafiri nje ya nchi ataweza kunufaika
Hii ni bima inayokulinda dhidi majanga ya kiuchumi, upotevu au uharibifu unaoweza kutokea ukiwa umesafiri nje ya nchi.
Akizungumza na HabariLeo Afisa Bima wa NIC, Hopegeorge Nganisa amesema bima hiyo inaweza kukupa fidia ya kucheleweshwa kwa vifurushi au mzigo wako,msaada wa kisheria kwa matukio kama kughairishwa au kufutwa kwa safari katika dakika za mwisho na matibabu ya dharura safarini, iwapo utafariki ukiwa safarini na iwapo umevamiwa na kupoteza fedha na nyaraka
“Unaweza kuchukua bima ya safari fupi kuanzia siku tano hadi saba, unaweza kuchukua ya mwezi mmoja au safari ndefu za kimataifa kwa miezi sita, mwaka inategemea na safari yako.”Amesema Nganisa na kuongeza
“Bima hii ni ya hiyari ingawa kuna baadhi ya nchi ni lazima uwe na bima hii ili kuweza kwenda kwenye inchi hizo.”Amesema
Aidha Nganisa ameshauri kuwa ni vyema mtu anaposafiri nje ya nchi kupata bima hiyo bila kujali ni kwa hiyari au ni kwa mujibu wa sheria ya nchi anayokwenda.
Amesema, bima hiyo ni gharama nafuu na itakupa amani ya moyo ukiwa safarini .
Comments are closed.