Onyo latolewa wanaochelewesha miundombinu ya shule

MOROGORO: KATIBU Mkuu Ofisi ya  Rais , Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) ,Adolf Ndunguru amewataka viongozi wa mikoa na halmashauri ambazo ujenzi  wa miundombinu ya shule haijakamilika wajitafakari wenyewe  kabla ya kuchukuliwa hatua za kinidhamu.

Ndunguru ,amesema hayo Januari 4, 2024  wakati akifungua kikao kazi cha Makatibu Tawala wasaidizi elimu mikoa na maofisa elimu wa halmashauri nchini mjini Morogoro

Aidha amesema  pamoja na dhamira  njema ya serikali kutekeleza miradi mbalimbali ya elimu, wapo baadhi ya viongozi ambao wameshindwa kusimamia na kukamilisha  utekelezaji wa miradi hiyo kwa muda uliopangwa .

Katibu mkuu huyo alitolea mfano kuwa ,ipo mikoa ambayo ujenzi wa miundombinu ya shule bado ipo chini ya asilimia 50, licha ya maelekezo ya serikali ya kuwataka kukamilisha ujenzi kabla ya Desemba 30, 2023.

Ndunguru ,ameongeza  kumekuwepo  na visingizo  na maelezo luluki kuhusu changamoto za kutokamilisha kazi hiyo  na sababu hizo   haziwezi kusaidia kwa wakati huu .

“ Kumbukeni kuwa wapo wenzenu wamekamilisha miradi hiyo huku wakiwa na mazingira magumu kuliko nyie mnaosuasua “amesema Ndunguru.

 

 

 

Habari Zifananazo

Back to top button