Osimhen atwaa tuzo mchezaji bora Afrika

BOLOGNA, ITALY - SEPTEMBER 24: Victor Osimhen of SSC Napoli looks on during the Serie A TIM match between Bologna FC and SSC Napoli at Stadio Renato Dall'Ara on September 24, 2023 in Bologna, Italy. (Photo by Alessandro Sabattini/Getty Images)

STRAIKA wa Napoli na timu ya taifa ya Nigeria, Victor Osimhen ameshinda tuzo ya mchezaji bora Afrika kwa wachezaji wanaocheza nje ya Afrika.

Katika tuzo hizo zinazotolewa leo na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF), Osimhen amewashinda Hachraf Hakimi wa Morocco na Mohamed Salah kutoka Misri.

Tuzo hiyo imetokana na ubora wa msimu uliopita wa mchezaji huyo ambapo akiwa Napoli alifunga mabao 29 katika michezo 38 ya Ligi Kuu Italia ‘Serie A’

Advertisement

Sambamba na kufunga mabao hayo, mkali huyo wa kucheka na nyavu aliifanikishia Napoli kushinda ubingwa wa ligi hiyo msimu uliopita.

Aidha kwa upande wa wanawake tuzo ya mchezaji bora imeenda kwa Asisat Osoala wa Nigeria akiwapiku Thembi Kgatlana wa Afrika Kusini na barbara Banda wa Zambia.

12 comments

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *