Wahimizwa kufanya tafiti zenye tija

MWANZA: WATAFITI nchini wametakiwa kufanya tafiti zenye tija na kuhakikisha matokeo ya tafiti hizo yanawafikia wananchi ili kuchangia utatuzi wa changamoto za jamii na kuchochea ukuaji wa uchumi wa taifa.

Rai hiyo imetolewa leo Novemba 25, 2025 jijini Mwanza na Mkaguzi Mkuu wa ndani wa Serikali, Benjamin Magai, katika uzinduzi Kongamano la Nne la Kimataifa la Usimamizi wa Biashara na Ukuaji wa Uchumi, linaloratibiwa na Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA).

Magai alisema kuna umuhimu mkubwa kwa watafiti kufanya tafiti zenye matokeo yanayoweza kutumiwa na watunga sera na wadau mbalimbali, ili kuwezesha maendeleo ya kijamii na kiuchumi kuendana na kasi ya mabadiliko ya dunia.

Naye, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania(TIA), profesa William Pallangyo amesema kongamano hilo ambalo linaendelea jijini Mwanza, limewakutanisha watafiti, wataalumu, wadau wa biashara na uchumi kutoka ndani na nje ya nchi, ikiwa ni mwendelezo wa jitihada za TIA kuimarisha tafiti, mafunzo na ushauri wa kitaalam tangu kuanzishwa kwa makongamano hayo mwaka 2022.

Amesema dhima kuu ya kongamano la mwaka huu ni Uvumbuzi, Ubunifu na Biashara kwa Uchumi Endelevu. Amesema kuwa baada ya majadiliano ya tafiti, taasisi hiyo itatayarisha kitabu maalum chenye mapendekezo ya kitaalam kuhusu namna bora ya kukabiliana na changamoto zilizobainishwa.

Habari Zifananazo

2 Comments

  1. JOIN US Everybody can earn 250/h Dollar + daily 1K… You can earn from 6000-12700 Dollar a month or even more if you work as a part time job…It’s easy, just follow instructions on this page, read it carefully from start to finish… It’s a flexible job but a good earning opportunity. tab for more detail thank you……..
    .
    This is my main concern……………………………………. http://Www.Cash43.Com

  2. Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
    .
    M­­­­­­o­­­­­­r­­­­­­e­ D­­­­­­e­­­­­­t­­­­­­a­­­­­­i­­­­­­l­­­­­­s For Us→→→→→→→→→→ http://Www.Payathome9.Com

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button