Polisi yaonya kugusa waliouawa, waliojiua

JESHI la Polisi limeonya wenye tabia ya kuingia katika maeneo ya matukio, kushika au kugusa vitu vilivyotumika katika uhalifu.

Pia limeonya kushika watu waliouawa au kujiua kabla ya uchunguzi na kuitaka jamii kuacha haraka tabia hiyo kwani kasumba hiyo, huharibu uchunguzi na kuwaingiza katika kesi za jinai na mauaji.

Kamishina wa Polisi (Operesheni na Mafunzo), Awadhi Juma alisema hayo Dar es Salaam alipozungumza na HabariLEO kuhusu kasumba ya baadhi ya watu kuingia maeneo ulipotendeka uhalifu na kushika vielelezo kabla ya uchunguzi wa polisi.

“Watu waepuke tabia hiyo kabisa maana inaharibu uchunguzi hasa katika kuchukua alama za vidole na pia.

“Inawafanya wawe hatarini kushitakiwa wakihusishwa na uhalifu au mauaji hayo kwa kuwa alama za vidole vyao zitaonekana badala ya alama za wahalifu pekee,” alisema Awadhi.

Akaongeza: “Yanapotokea matukio ya kihalifu, watu wasiingilie eneo husika hadi polisi watakapofika na kumaliza uchunguzi wao; ukifanya hivyo, utaharibu uchunguzi na unaweza kuharibu ushahidi na hata kuhusishwa katika uhalifu huo”.

Awali katika banda la Polisi lililopo katika Maonesho ya 47 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam katika Viwanja vya Julius Nyerere vilivyopo Temeke Dar es Salaam, Sajenti Samson Kasongi wa Kamisheni ya Uchunguzi wa Kisayansi wa Polisi makao makuu alisema katika maeneo mbalimbali polisi wanashindwa kupata taarifa sahihi.

Alisema pia wanakosa taarifa za kutosha kutokana na watu kuingia na kushika vielelezo zikiwamo silaha zilizotumika na kubaki au vitu vilivyoathirika au kudondoshwa katika tukio hilo la uhalifu.

“Kwenye tukio la mauaji, wananchi msishike wala kukanyaga vitu ili msiingizwe katika uhalifu huo badala yake, toa taarifa ili polisi waje na kukusanya taarifa muhimu za uchunguzi,” alisema Sajenti Kasongi.

Akaongeza: “Ukikuta mtu kauawa, usianze kumgusa au kushika vitu vilivyopo hapo kuonesha watu, subiri polisi waje ili usijiingize kwenye matatizo yasiyokuhusu”.

Msaki Theobald wa Kitengo cha Uchunguzi wa Matukio ya Kihalifu katika Jeshi la Polisi alisema katika maonesho hayo kuwa, polisi wanatoa hadhari hiyo kwa kuwa wahalifu wanaweza kuua mtu, kisha wakamning’iniza kama mtu aliyejinyonga na kuacha ujumbe ili kupotosha uchunguzi.

“Sisi hatuishii kuona amening’inia kuwa amejinyonga na eti tukaona karatasi ameacha ujumbe tukaamini hapana, tutafanya uchunguzi wa kina kwa vitu vyote vilivyohusika na kutumika mfano, kwenye kamba tutaangalia kama kuna vidole vya mtu mwingine au ni yule aliyekufa na hata hiyo karatasi, tutaichunguza,” alisema.

Akaongeza: “Tunaweza kuona kama kweli ndiye aliandika kabla hajafa, au imeandikwa na waliomuua hivyo, ukishika vitu hivyo, vidole vyako vitaonekana na wewe utahusishwa na mauaji hayo”.

Kumekuwa na matukio ya watu kukutwa wamekufa kwa kinachodaiwa kuwa ni kujinyonga huku wengine wakiacha ujumbe wa maandishi unaohusu sababu zake kujitoa uhai.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
4 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
kirdilipsu
kirdilipsu
2 months ago

Google now pays $99 to $140 per hour to do online work from home jobs. My last paycheck said $18537 from this easy and simple job. It’s amazing and winning is awesome. No boss, full time freedom and profits are ahead of you. This work is just awesome. Any person can make income online with google easily
.
.
.
HERE========= ►► https://fastinccome.blogspot.com/

MaryRoss
MaryRoss
2 months ago

S­t­a­r­t w­o­r­k­i­n­g f­r­o­m h­o­m­e! G­r­e­a­t w­o­r­k f­o­r-E­v­er, ­S­t­a­y a­t H­o­m­e M­o­m­s O­R a­n­y­o­n­e n­e­e­d­s­ a­n e­x­t­r­a i­n­c­o­m­e. G­e­t s­t­a­r­t­e­d. Y­o­u o­n­l­y n­e­e­d­ a bgh computer a­n­d a reliable c­o­m­p­u­t­e­r c­o­n­n­e­c­t­i­o­n­ s­o d­o­n’t g­e­t l­a­t­e t­r­y……. https://workscoin1.pages.dev/

Last edited 2 months ago by MaryRoss
Drinnera1939
Drinnera1939
2 months ago

Making an extra $15,000 per month from home by doing easy copy and paste type internet work. I earned $18,000 from this simple at-home job. Everyone may now easily generate additional money online.
.
.
Detail Here————————>>> http://www.dailypro7.com

Julia
Julia
2 months ago

Work from home and get money. You have the option of working from home anytime you choose. Working only 5 hours per day online, you might earn more than $600 each day. In my leisure time, I made $18,000 using this.
.
.
Detail Here——————————————————–>>>  http://Www.OnlineCash1.Com

Back to top button
4
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x