JUHUDI, bidii, ari ya kujitolea imetajwa kuwa miongoni mwa sababu zilizowapa Yanga ubingwa wa Ligi Kuu Bara msimu wa 2022/2023.
Rais wa FIFA, Gianni Infantino amesema hayo kupitia barua iliyotolewa leo na Shirikisho la Soka (TFF).
Katika taarifa hiyo Infantino ameipongeza Yanga kwa kutwaa ubingwa huo sambamba na waliohusika katika safari hiyo ya mafanikio.
Rais huyo ameipongeza pia TFF kwa mchango wake katika maendeleo na ustawi wa soka la Tanzania na Afrika.