Rais Hungary kuwasili Tanzania leo

RAIS wa Hungary, Katalin Novak anatarajiwa kuwasili leo na kufanya ziara yake nchini Tanzania kuanzia leo Julai 17 mpaka Julai 20 ,2023. Ziara hiyo ni matokeo ya jitihada  ya Rais samia suluhu hassan za kuimarisha uhusiano wa kidplomasia na mataifa mengine.

Waziri wa  Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk Stergomena  Tax amesema kufanyika kwa ziara hiyo ni vipaumbele vya Rais  Samia katika kuimarisha uhusiano wa kimataifa na  kikanda.

Kamishna wa Kitengo cha Fedha za Nje kutoka Wizara ya Fedha, Rished Bade amesema katika ziara hiyo na Rais Katalini watajadili juu ya uwekezaji wa kilimo, utangazaji na uzalishaji wa bidhaa mbalimbali ili kuendelea kuimarisha uhusiano.

Advertisement

Mkurugenzi wa Kitengo cha Habari Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mindi Kusiga amesema ziara hiyo imekuja kutokana na sera mpya  nchini Hungary Kwa nchi za Afrika inayolenga Kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi ambao ulianza kutekelezwa  na Taifa hilo miaka michache iliyopita.

 

5 comments

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *