Rais Liberia kuangalia upya sekta ya madini

RAIS mteule wa Libeŕia, Joseph Boakai, ambaye alimshinda Rais George Weah amesema utawala wake utaangalia kwa makini maafikiano ya uchimbaji madini ili kuhakikisha yananufaisha nchi hiyo.

“Hatua ya kwanza ya kuikomboa Libeŕia ni kuichukua kutoka kwa watu hawa. Imeokolewa. Jambo linalofuata ni kushughulikia masuala ambayo yanatanda katika nchi hii,” Boakai alisema, akitoa mfano wa ŕushwa na ukosefu wa huduma za msingi.

Boakai alisema eneo muhimu ambalo Waliberia hawajanufaika nalo ni sekta ya madini, licha ya kuwa na akiba ya madini nchini Libeŕia, ikiwa ni pamoja na almasi, dhahabu, chuma na mbao.

Alipoulizwa kama hii itajumuisha kupitia upya mikataba ya uchimbaji madini, Boakai alisema mapitio yatafuatiliwa iwapo itathibitishwa.

Boakai alimshinda Wear katika duru ya pili ya uchaguzi wa Rais wa Novemba 14, 2023, ambapo mpinzania wake huyo alikubali kushindwa na kumpongeza.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
1 Comment
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
RubyHutcherson
RubyHutcherson
17 days ago

I’ve gained only within four weeks by comfortably working part-time from home. Immediately when I had lost my last business, mtg I was very troubled and thankfully
following website___________ http://Www.Careers12.com

Last edited 17 days ago by RubyHutcherson
Back to top button
1
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x