Rais Malawi aomba msaada

Malawi's President Lazarus Chakwera delivers a speech at the leaders summit of the COP27 climate conference at the Sharm el-Sheikh International Convention Centre, in Egypt's Red Sea resort city of the same name, on November 8, 2022. (Photo by AHMAD GHARABLI / AFP)

RAIS wa Malawi, Lazarus Chakwera ameomba msaada kwa mashirika ya misaada ya kimataifa kufuatiwa uharibifu wa makazi ya watu uliotokana na kimbunga freddy kilichouwa watu 225.

Akizungumza jana jioni katika mji Mkuu, Blantyre Rais Chakwera amesema janga hilo limerudisha nyuma maendeleo ya watu kwa kiasi kikubwa na kuziomba Jumuiya za Kimataifa kuwapa misaada mbalimbali ya chakula, mavazi na malazi.

“Malawi iko katika hali ya maafa. Kile kimbunga Freddy amefanya, ni kuturudisha nyuma hata tulipokuwa tunajaribu kujenga upya, kwa sababu ya majanga yaliyopita. Na ninaomba jumuiya ya kimataifa ituangalie kwa upendeleo kama huo. tunahitaji msaada”.alisema Chakwera.

Advertisement

Ilikuwa ni mara ya pili ndani ya wiki tatu kwa nchi hiyo kukumbwa na kimbunga Freddy ambacho pia kiliathiri nchi jirani ya Msumbiji.

Watu wengi waliangamia katika maporomoko ya ardhi yaliyosomba nyumba dhaifu zilizojengwa kwenye miteremko.

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *