RAIS Kikwete amesema “Nimemfahamu Membe miaka mingi, tumetoka nae mbali na tumesaidiana kwa mengi, familia zetu, na mapito ya maisha yetu yamehusiana sana, Bernard Kamillius Membe alikuwa ni mtu wa msaada mkubwa kwangu katika maisha yangu ya kikazi na kisiasa.
”

” Amesema na kuongeza
“Nautambua mchango wake mkubwa alioutoa kwenye Chama Cha Mapinduzi alipokuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Mjumbe wa Kamati Kuu na Katibu wa Siasa na Uhusiano wa Kimataifa katika Sekretariati ya Halmashauri Kuu ya Taifa, katika nafasi zote hizo, alijitoa kwa moyo wake wote na kuacha alama za Kudumu.

“Hakika Taifa limepoteza mmoja wa watu wake muhimu, natoa salaam za rambirambi na mkono wa pole kwako Shemeji yangu Dorcas Membe na Watoto wenu Cecilia, Richard na Dennis, pamoja na Wajukuu, ndugu na jamaa wa marehemu Bernard Kamilius Membe, nawapeni pole kwa msiba mkubwa uliowakuta.
