Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ameshuhudia utiaji saini wa mikataba mitatu ya msaada wa Sh bilioni 455.09 kutoka Umoja wa Ulaya (EU).
Fedha hizo zitatumika kuimarisha mifumo ya usimamizi wa fedha za serikali na kukuza sekta binafsi, uchumi wa buluu na kuimarisha uhusiano kati ya Umoja wa Ulaya na Tanzania katika kuongeza ufanisi kwenye kubuni na kusimamia miradi inayofadhiliwa na EU.