Rais Samia atoa Sh milioni 10 kwa wavuvi waliofanya uokoaji

Shughuli uwanja wa Kagera zarejea

RAIS  wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania  Samia Suluh Hassani, ametoa  shilingi Milioni 10 kwa wavuvi wa Mwalo wa Nyamukazi ambao walishiriki kufanya uokoaji wa abria katika ajali ya ndege ya Precision iliyotokea Novemba 6 mwaka huu na abiria  19 kupoteza maisha

Mkuu wa Mkoa wa  Kagera Albert Chalamila na maofisa mbalimbali kutoka ofisi ya Waziri Mkuu  walifika katika Mwalo wa Nyamukazi na kukutana na wavuvi ambao wameomba kujipangia matumizi juu ya fedha hizo.

Chalamila amemtaka kufunguliwa akaunti maalum ya kuweka fedha hizo ili wavuvi walioshiriki kufanya uokoaji waweze  kupanga mikakati ya namna watakavyotumia fedha hizo na namna zitakavyowasaidia .

Hata hivyo shughuli katika uwanja wa ndege wa Bukoba zimerejea kama awali hivyo ratiba ya ndege kutoka katika makampuni mbalimbali kutua na kuondoka inaendelea.

 

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button