Rais Samia awapa maelekezo mabalozi

RAIS Samia Suluhu Hassan amewataka mablozi wateule  kujifunza zaidi jinsi mataifa mengine yanavyofanya katika ukuaji wa uchumi wa mataifa yao, ili wahamishie ujuzi huo nchini, kwani kazi yao sio kufanya uwakilishi tu wa Tanzania katika mataifa hao.

Akizungumza mara baada  ya uapisho wa mabalozi hao aliowateua, Rais Samia amesema wapo mabalozi ambao wanaonekana  pale ambapo ujumbe wa Tanzania umekwenda kwenye nchi hiyo, anapokea wageni, anawasindikiza , au Watanzania wafanye ukorofi ndio utaona ripoti ya balozi, au unamuona siku za sherehe za kitaifa za nchi hiyo, lakini mengine hakuna, hakuna la maana linalotoka huko.

“Katika nchi nyingine mabalozi wetu sijui niseme hawajui wanachokifanya, wapo tu. Nilikutana na Rais mwenzangu ndani ya SADC akaniambia nimbadilishie balozi kwa kuwa aliyepo kazini haendi na mikutano hashiriki.

“Sasa nyinyi nataka mkafanye kazi, mtuambie wenzetu wamefanya uchawi gani kukua kiuchumi na sisi tunakosa nini, tuna rasilimali hatuzitumii? Au kitu gani, ila niseme wazi wenzetu wamepiga hatua kubwa sana licha ya kuwa sisi tumewazidi kwenye rasilimali, diplomasia ya uchumi ifanye kazi hapa, tujiulize tuliachwa wapi?”Amehoji.

Rais Samia  ameiagiza Wizara ya Mambo ya Nje kuweka mfumo utakaoonesha kazi zote zinazofanywa na balozi za Tanzania katika mataifa mbalimbali, huku akihimiza matumizi ya TEHAMA katika kurahisisha na kuharakisha kazi.

Mabalozi walioapishwa leo na nchi wanazokwenda kwenye mabano ni  Fatma Mohamed Rajabu kuwa Balozi wa Tanzania nchini Omani, Joseph Sokoine (Canada), Naimi Hamza Azizi (Austria).

Meja Jenerali Ramson Mwaisaka (Rwanda), Meja Richard Makanzo (Cairo Misri), Gelasius Byakanwa (Burundi), Habibu Awesi Mohamed (Qatar) na Mahadhi Juma Maalim (Kuala Lumpur, Malaysia).

Pia wapo Imani Njalikai (Algeria), Hassan Idd Mwamweta (Ujeruamani),  Abdallah Saleh Posi (Geneva, Uswisi)  Dk Mohamed Juma Abdallah (Saudi Arabia) na Jabir Mwadini (Ufaransa).

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
5 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
yirzoharde
yirzoharde
1 month ago

My first payment is $27,000. I’m thrilled since this is the first time I’ve truly earned stuff. From this point on, I’m going to work even harder, and I can’t wait till the next vs10 week to get paid. Click the home tab to find out more.
.
.
Using Here————————————>> https://fastinccome.blogspot.com/

MAPINDUZI YA ELIMU
MAPINDUZI YA ELIMU
1 month ago

WAZO JADIDIFU UKIONA WEKAZO HAWAFANYI KAZI KAMA RAIS WA TANZANIA (HAFANYI KAZI VIZURI KABISA) NA UNATAKIWA UPINDUE NCHI UTATUMIA CHOMBO GANI CHA HABARI… MAPINDUZI YA KIJESHI MATHARANI KUTAKUA NA RAIS AJAE KAMA MKAPA HUKO
·        THE GUARDIAN,
·         THE CITIZEN,
·         MWANANCHI,
·         DAILY NEWS,
·        NIPASHE,
·        TBC TAIFA,
·         RFA,
·        RADIO ONE,
·        CLOUDS FM,
·        TBC1,
·        ITV, NA
·        AZAM TV.

MAPINDUZI YA ELIMU
MAPINDUZI YA ELIMU
1 month ago

WAZO JADIDIFU UKIONA WEKAZO HAWAFANYI KAZI KAMA RAIS WA TANZANIA (HAFANYI KAZI VIZURI KABISA) NA UNATAKIWA UPINDUE NCHI UTATUMIA CHOMBO GANI CHA HABARI… MAPINDUZI YA KIJESHI MATHARANI
·        THE GUARDIAN,
·         THE CITIZEN,
·         MWANANCHI,
·         DAILY NEWS,
·        NIPASHE,
·        TBC TAIFA,
·         RFA,
·        RADIO ONE,
·        CLOUDS FM,
·        TBC1,
·        ITV, NA
·        AZAM TV.

MAPINDUZI.GIF
Najma
Najma
1 month ago

huyu demu aliyecheza na diamond JEJE MZURI SANA ANAPATIKANA MKOA GANI ANATAFUTWA… TUMPE MAUA YAKE ANASTAHILI KUWA NA WAJUKUU 90… NAENDA KUJENGA HOTEL KWA SABAU YAKE

OIP.jpeg
Chukua Mkifo huooo
Chukua Mkifo huooo
1 month ago

Matokeo yanaonesha ya Majengo+Mlinzi yanayotakiwa kusikimikwa viwanda/ viliyofunguliwa zamani ni 455,789 vinasubiri wawekezaji wapya kabisa kutoka labour

Matokeo yanaonesha kuwa, katika jumla ya viwanda vyote 49,243 (vikubwa na vidogo) vilivyohusika katika Sensa ya Uzalishaji Viwandani kwa mwaka 2013.

MAPINDUZIII.GIF
Back to top button
5
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x