RC Moro aipongeza Fountain Gate

RC Moro aipongeza Fountain Gate

MKUU wa Mkoa wa Morogoro, Fatma Mwassa  ameipongeza menejimenti ya shule ya Fountain Gate kwa kuwaandaa vizuri vijana wao, wakiwemo wa timu ya wasichana wa mpira wa miguu  na kutwaa ubingwa wa Mashindano ya Shule ya Afrika.

“ Naipongeza timu yetu Fountain Gate kwa kufanya vizuri, lakini wakati mnapita kwenda Dodoma mkawiwa  kutusalimu sisi wa Morogoro na hii ni kwa sababu mfugaji bora ni mzaliwa wa Morogoro, mkasema mtupitishie na sisi tuipongeze timu na pia kumpongeza mwana Morogoro na mwalimu anayewafundisha anatokea pia Morogoro, “ amesema Mwassa.

Advertisement

Ameupongeza  uongozi wa Fountain Gate kwa kuwa na nia ya kuwekeza shule ya  sekondari ya kuinua vipaji mkoani Morogoro na kwamba  serikali ya mkoa itatoa ushirikiano  kwa kuhakikisha ndoto hiyo inatimia .

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *