Serikali bega kwa bega na sungusungu

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga, Christina Mndeme amesema serikali itaendelea kulisimamia jeshi la jadi maarufu ‘sungusungu’ nakulishauri sababu linasaidia suala la ulinzi na usalama pamoja na kuhamasisha maendeleo.

Mndeme amesema hayo jana alipokuwa mgeni rasmi katika mkutano mkuu wa sungusungu kwa Kanda ya Ziwa uliokutanisha mikoa mitatu ya Simiyu, Mwanza na Shinyanga nakufanyika kijiji cha Busanga wilayani Kahama.

Mndeme akiwa mshauri na mlezi wa sungusungu ndani ya mkoa huu aliwataka  sungusungu  kushiriki  kulinda miradi ya maendeleo inayotekelezwa na serikali  maeneo yote.

Mndeme amesema  jeshi la jadi liendelee kulinda  amani iliyopo  ili isipotee na kuwaepuka watu wenye nia mbaya  na kupinga vitendo vya ukatili kwa wanawake na watoto.

Mndeme amesema serikali katika mkoa wa Shinyanga imeleta jumla ya Sh trilioni 1 kutekeleza miradi ya maendeleo na uendeshaji wa sekta mbalimbali.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Work At Home
Work At Home
1 month ago

My last pay check was $9500 working 12 hours a week online. My sisters friend has been averaging 15k for months now and she works about 20 hours a week. I can’t believe how easy it was once I tried it out. 

This is what I do…. http://Www.Smartcash1.com

Last edited 1 month ago by Work At Home
Back to top button
2
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x