Serikali yatoa tamko, kuhamisha wananchi Ngorongoro

DODOMA: Serikali imesema siku chache zijazo itaendelea na awamu ya pili ya shughuli ya kuwahamisha kwa hiari wananchi wa Tarafa ya Ngorongoro wilayani Ngorongoro mkoani Arusha, wanaoishi ndani ya Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro.
Akitoa taarifa hiyo leo Desemba 15, 2023 Msemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema shughuli hiyo ni kwa wananchi waliotayari na waliokwisha kujiandikisha.
“Serikali inarudia kusisitiza tena, zoezi hili ni la hiari na hakuna haki za binadamu zinazovunjwa na linafanyika kwa faida ya wananchi wenyewe ambao ni raia wa Tanzania wanaostahili usalama na maendeleo pamoja na hifadhi ambayo ni urithi wa taifa hili na dunia nzima.
Aidha ameongeza kuwa Serikali inasisitiza pia wananchi wa Wilaya ya Ngorongoro waliopo Lolindo hawafukuzwi kwenye maeneo yao bali serikali ilikubali kuwaachia eneo la Km za mraba 2,500 na kubakia na Km za mraba 1,500 ambazo ni kwa ajili ya hifadhi ya misitu, vyanzo vya maji, wanyama na ni sehemu muhimu ya mfumo wa ikolojia wa Serengeti na Maasai Mara unaojumuisha mzunguko wa wanyama – kuhama kwa wanyama.
Matinyi amesema kuwa Serikali iko tayari kuwapokea wataalamu wa UNESCO wanaokuja kuangalia jinsi zoezi hili linavyokwenda ikiwemo kukagua uhifadhi wa Ngorongoro.
“Wataalamu hawa watakuja Januari 2024. Serikali inatambua kwamba jumuiya na asasi mbalimbali za nje ya nchi zinaweza zikatoa maoni yao kwa kadri zinavyofahamu lakini ni muhimu wahusika wote wakatafuta ukweli ikiwemo kuja nchini kwa kupanga vema na serikali. Serikali ina uhusiano mzuri na EU na hivi karibuni Kamishna wa EU, JANEZ LENARCIC, aliielezea Tanzania kama mshirika wa kimkakati na ushirikiano uliopo baina ya Tanzania na EU unaendelea kuimarika” amesema Msemaji Mkuu wa Serikali.
180573 908894This plot doesnt reveal itself; it has to be explained. 385867
457520 586394You created some decent factors there. I looked on the internet for the dilemma and found most individuals will go along with together with your site. 990751
183077 534210I actually like your writing style, fantastic information, thankyou for posting : D. 663207
173330 800787You produced some decent points there. I looked online to the issue and discovered a lot of people is going in addition to making use of your web site. 588685
420381 683538I real delighted to find this site on bing, just what I was searching for : D also bookmarked . 510057
387908 377146Wonderful post, thank you so considerably for sharing. Do you happen to have an RSS feed I can subscribe to? 283293
396438 250324Im not that a lot of a internet reader to be honest but your blogs actually good, keep it up! Ill go ahead and bookmark your internet site to come back down the road. Cheers 138488
888944 822266A weblog like yours really should be earning much dollars from adsense.~::- 650818