Serikali yaweka mkakati kutatua mgogoro wa miaka 20

GEITA: SERIKALI kupitia Wizara ya Madini imeweka mkakati wa kuhakikisha inatatua mgogoro wa muda mrefu uliodumu zaidi ya miaka 20 tangu kuanza kwa shughuli za uchimbaji madini kati ya wananchi na mgodi unaomilikiwa na Kampuni ya Geita Gold Mine (GGM).
Akizungumza Waziri wa Madini Anthony Mavunde mkoani Geita alipofanya ziara ya kikazi kutembelea maeneo yenye mgogoro wa vigingi na mipasuko baina ya wananchi na mgodi wa GGM amesema mgogoro huo umedumu kwa muda mrefu kitu ambacho sio kizuri.
“Kipekee kabisa, naomba nimshukuru kwa dhati mtangulizi wangu ambaye kwa sasa ni Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mheshimiwa Dk. Doto Biteko kwa kazi nzuri ambayo alishaianza katika jambo hili.
.
“Kupitia kazi yake, imenifanya mimi kupata mahali pa kuanzia na kazi yangu kuwa nyepesi kuelekea kupata ufumbuzi wa mgogoro huu.” Amesema Mavunde.
Katika maeneo yote ya Nyakabale, Nyamilembo, Samina na Katoma alikotembelea, Mavunde alibainisha kwamba amepata fursa ya kuona hali halisi ya mgogoro huo, na kuahidi kutufanyia kazi na kufika mwisho.
Aidha, Mavunde amesema maoni ya Kamati ya Wataalam, Kamati ya wananchi na GGM alikwisha yaona, aliona ni jambo jema yeye mwenyewe kufika kujionea hali halisi kabla ya kufanya maamuzi ya mwisho.
I’ve gained only within four weeks by comfortably working part-time from home. Immediately when I had lost my last business, mtg I was very troubled and thankfully
following website___________ http://Www.Careers12.com
★ Join this most wonderful and cool online home based job and start making more than $700 every day. ( y01q) I made $24583 last month, which is incredible, and I strongly encourage you to join and begin earning money from home. Simply browse to this website now for more information.
Click and Copy Here══════►►► http://Www.SmartCareer1.com