ALIYEKUA Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Shaka Hamdu Shaka, amemkabidhi ofisini Sophia Mjema.
Shaka, amemkabidhi ofisi ikiwa ni siku chache baada ya Mkutano Maalum wa Halmashauri Kuu ya CCM, chini ya Rais Samia Suluhu Hassan kumteua Mjema kuchukua nafasi ya Shaka.
Makabidhiano hayo yamefanyika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Lumumba, Dar es Salaam.