Shibula yashinda 2-1 dhidi ya Bezi

KATA ya Shibula imepoteza kwa mabao 2-1 dhidi ya Bezi katika mchezo wa kundi D kwenye mashindano ya Angeline Jimbo cup uliochezwa leo katika uwanja wa shule ya msingi Bugogwa mkoani Mwanza.
Mabao ya Bezi yalifungwa na Mamba Juma dakika ya 35 na Denis Fungo dk ya 66.
Mpaka mapumziko timu hizo zilikuwa 1-1.
Katika uwanja Kona ya Bwiru,Kirumba ilishinda kwa bao 1-0 dhidi ya Kitangiri. Kwenye uwanja wa shule ya sekondari Buswelu,Nyakato ilishinda kwa mabao 2-1 dhidi ya Mecco.
Kwenye uwanja wa shule ya msingi Sabasaba,Nyasaka ilishinda kwa mabao 3-0 dhidi ya Kawekamo.