Shimiwi yashika kasi Tanga
MASHINDANO ya Michezo ya Wizara na Idara za Serikali (Shimiwi) yameendelea kushika kasi mkoani Tanga.
Katika michezo iliyofanyika leo, timu ya netiboli ya Bunge iliifunga Tarura mabao 16-11, wakati mpira wa miguu Bunge na Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari zilitoka sare ya kufungana bao 1-1.



